13/05/2026
NYUMBA ZA KUFICHA BATI NI NZURI ILA MPAKA UKUTANE NA MAFUNDI WANAOJUA WANACHOKIFANYA
Habari za leo maboss zangu k**a ulivyosoma hapo juu , kwenye kichwa
cha habari tofauti iliyopo kati ya nyumba ya kutokeza paa na nyumba ya kuficha paa nitawaelezea japo kwa kifupi.
1) Nyumba za kuficha paa
Nadhani kwa dunia ya leo akuna , asiyejua nyumba hizi za kuficha paa,
sio kwamba hazikuwepo zilikuwepo toka miaka ya themanini ila tofauti yake miaka ya themanini ni maji
yalikuwa yanamwaga nyuma kwa na Kwa mbele ( kutambele kunawekwa
tofali na kutambili za pembeni ( kuta 3)kasoro nyuma ambapo kunakuwa wazi bati linakuwa linapitisha maji
_Miaka ya leo zinavyojengwa zimekuwa na utofauti ndio zinapooneka kuwa ni nyumba za kisasa
Kutazote 4 zinaficha paa linakuwa alionekani na katikati ya nyumba
kunakuwa na mfereji wa kupitisha maji , au pembeni mfereji wa maji na kunakuwa na cover za kuzuia maji
yasipenye kwenye ukuta na kuna matilio kutoka kampuni ya sika yanayouzuia maji kupenya kwenye ukuta.
Kwenye mfereji lazima kuwekwe flaw na materials ya kuzuia maji yasipenye yapo matilio hayo kutoka kampuni ya
sika na juu yake kuwekwe tiles ili kuwezesha maji kulilika kwa speed mbaka kwenye bomba la kupokea maji kupelekea chini.
_faida na shida zake nyumba za kuficha paa.
a) faida ya nyumba ya kuficha paa japo kwa ufupi
_ Kipindi cha upepo mkali ( kimbunga) kwa kuwa bati limejificha swala la paa kun'goka halitotokea kwenye nyumba hizi
_ Kwa kuwa paa limejificha unaweza kuweka bati la ainayeyote na nyumba ikawa imependeza( ila tunapendeka liwe la gage 28) Kwa nyumba inakuwa imeficha paa
_ Mfumo wa kuficha paa unakula bati chache na mbao chache wakati wa Kupaua
a) Shida za nyumba ya kuficha paa
_ K**a ukishindwa kutafuta fundi usiyekuwa na taarifanaye hizi nyumba zinasumbua kuvuja
_ Asikuongopee mtu kwamba izi nyumba zinapunguza gharama hapana . Hizi nyumba Jenga Kwa kupenda azipunguzi gharama.
b) Nyumba za kuonekana paa
(a) Faida ya nyumba za paa la kutokeza japo kwa ufupi
_ Bati linafunika nyumba nzima na kupelekea kuta kutoweza kuloa.
_ Bati linakaa miaka mingi zaidi bila kuisha( kuchakaa)
_Tatizo la nyumba kuvujisha halipo la umpate fundi usiyekuwa na taarifanaye
b) Hasara ya paa kutokeza japo kwa ufupi .
_Vifaa upande wa bati,mbao vinatumika vingi.
_ Kwenye mazingila ya hali ya hewa kuwa mbaya ( upepo mkali) paa linawezekana likatoka
_ Kwa kua paa linaoneka hata ikitokea umeweka bati mbaya hata muonekano wa nyumba unaonyesha.
📞📞wasiliana na sisi k**a nyumba yako ilipauliwa ila inavuja, k**a unataka kuanza au ushaanza ujenzi wa nyumba yako.
0766219197.