REAL Aquaculture group

REAL Aquaculture group REAL Aquaculture Tanzania Ltd
deals with
*Construction of Aquaculture infrastructure
*Pond management
*manufacturing of fish feed

14/10/2017

Habari yako, tuambie unafuga samaki gani na unakabiliwa na changamoto zipi ili tuweze kuzitatua kwa pamoja

21/02/2017

Habari za wakati huu,
je! unatatizo lolote linalokusumbua juu ya ufugaji samaki?.

Tuandikie ili tuweze kulitatua pamoja. karibu sana

11/12/2016

habari zenu
kuna mwenzetu Bw. John anachangamoto mbili na nasisi tunapenda kusshirikiana naye. HAta wewe k**a unaweza kuchangia ili tuboreshe na tuweze songa mbele. changamoto zake ni k**a zifuatavyo;

1. ukosefu wa maji ya kutosha
unapofikilia kufuga samaki, kuna vitu vitatu lazima uanze kwa kufukilia kwanza, lakini kimoja wapo

(a) upatikanaji wa maji bora na yakutosha; hii ni kwasababu samaki hutegemea maji kwa maisha yake yote yaani hutegemea maji kwa ajili ya upumuaji, kula chakula na kuishi. hivyo bila maji huwezi fuga samaki, na k**a utakuwa unayatoa mbali basi unaweza ukawa unaingia gharama kubwa sana. katika hatua za mwanzo za kuchagua eneo la kufugia samaki, upatikanaji wa maji ni jambo la kwanza kufikilia.

2. kasi ndogo ya ukuaji wa samaki.
kuna sababu mbalimbali ambazo zinaweza kufanya samaki yeyote asiweze kukua vizuri

(a) kupandikiza vifaranga kwenye bwawa
wazalishaji wa samaki wakati mwingine hutuuzia fry na sio fingerling. hii kwa maana ya kwamba, samaki anapoanguliwa kutoka kwenye yai anaitwa fry na anatakiwa kutunzwa na mzalishaji samaki mpaka anapofikia hatua ya fingerling (mwezi mmoja na nusu hadi miwili) na fingerling huwa na 10-20 g. fry hupewa chakula chao maalum ambacho kina kiasi kikubwa cha protein ili wakue vizuri. k**a ukinunua fry hivyo hawatapata special diet yao hivyo tegemea na ukuaji wao utakuwa suasua.

(b) chakula bora
hata samaki anahitaji chakkula bora na sio bora chakula ili aweze kukua vizuri. k**a chakula chako hakitakuwa na virutubisho vinavyohitajika na vyakutosha basi samaki wako hawataweza kukua vizuri.

(c) management
k**a hutakuwa unahudumia bwawa lako vizuri kwa maana ya kubalisha maji na kutoayanapochafuka huduma zingine basi ukuwaji wa samaki wako uatakuwa sio mzuri

(d) stocking density
k**a umewajaza samaki wengi kwenye bwawa lako bila kuangalia resources available kwenye bwawa lako basi usitegemee miujiza ya ukuaji wa samaki. uwekaji wa samaki kwenye bwawa (idadi) hutegemeana na ukubwa wa bwawa lako, pia hutegemea uwezo wako wa kuwahudumia hao samaki.

hizo ni baadhi tu ya sababu

03/12/2016

Habari
tafadhali tuelezee changamoto unazokutana nazo katika ufugaji wa samaki ili tuweze kuzitatua kwa pamoja

18/10/2016

Habari za leo,
kuna mmoja wetu ameuliza ni jinsi gani utatambua kuwa kunaugonjwa ndani ya bwawa lako na aina gani ya ugonjwa?

1. kwanza ni vyema kujua kuna aina 2 kuu za magonjwa
a). magonjwa yanayoambukizwa
b). magonjwa yasiyoambukizwa

a). magonjwa yanayoambukizwa
haya ni magonjwa yanaosababishwa na vimelea fulani na yamegawanyika katika sehemu tatu (3)

i).yanasababishwa na bakteria
ii). yanasababishwa na fangasi
iii). yanasababishwa na virusi

kila aina ya ugonjwa huonyesha dalili zaki kwa kila aina ya samakiwanayoshambulia. mengine yanakuwa na dalili za moja kwa moja ambao zinaonekana na rahisi kuzigundua. mf. bakteria wengine huanza kushambulia sehemu za nje za mwili ambapo humsababishia samakimuwasho. hivyo samaki wengi huanza kuogelea huku wakijisugua ukutani mwa bwawa, na wakati mwingine huruka juu ili kupata msuguano/ kujikuna. lakini mtu muhimu kugundua hali tofauti ya samaki ni yule anayewalisha kila siku. pindi anapoona samaki hawali k**a awalibasi ni vyema kutoa taarifa kwa mtaalam ili aweze kuja kuwaona na kutoa ushauri nini cha kufanya.

b). magonjwa yasiyoambukizwwa
haya yanasababishwa na upungufu wa baadhi ya virutubisho ndani ya mwili. hii inachangiwa na kulisha chakula ambacho hakina ubora/mahitaji muhimu ya virutubisho kwa samaki. aina tofauti tofauti ya samaki na stage mbalimbali za ukuaji wa samaki hutofautiana katika mahitaji ya virutubisho katika milo yao. sio bora chakula ila chakula bora kinahitajika kwa ukuaji wa samaki wako.

kushindwa kuwalisha samaki chakula bora huweza kudumaa, kupata magonjwa mengine ambayo yanaweza kumfanya asikue vizuri.

wakati mwingine ni vigumu sana kugundua amaki anaumwa ugonjwa gani, lakini kwa kuangalia feeding habit- ulaji wa chakula unaweza gundua kuwa samaki wako wana shida hivyo uwasiliana na wataalam kwa ushauri zaidi.

ubora wa maji ndani ya bwawa, aina ya ulishaji wa chakula, usafii wa vifaa vinavyotumika ndani ya bwawa na usafi wa mazingira kuzunguka bwawa ni mambo ambayo yanaweza kusababisha magonjwa kwa kiasi kikubwa.

09/10/2016

Je! wapenda kujua nini juu ya ufugaji samaki?.
Niandikie halafu tutashirikiana na wenzangu kukujuza.
Karibu sana

24/07/2016

MAGONJWA YA SAMAKI

Leo tutajifunza magonjwa ya samaki, na ili kiumbe chochote kiugue ugonjwa fulani, lazima kuwe na visababishi (vimelea) kisababishiwa (mnyama/samaki) na mazingira mazuri. Ili visababishi viweze kumdhuru samaki, lazima viwe vingi kushinda kinga ya samaki husika. Mazingira lazima yawe mazuri ya kuwezesha vimelea kusababisha ugonjwa 

1. magonjwa yanayoambukizwa
kuna magonjwa mbalimbali yanayoshambulia samaki na huambukizwa kutoka kwenye samaki mmoja hadi mwingine. Magonjwa hayo ni k**a ifuatavyo

a). Magonjwa yanayosababishwa na Bakteria
b). magonjwa yanayosababishwa na fangasi
c). magonjwa yanayosababishwa na virusi

2. Magonjwa yasiyoambukizwa
a).magonjwa yanayosababishwa na upungufu wa virutubisho mwilini

15/07/2016

Je!, wajua magonjwa ya samaki?.


30/06/2016

unatakufuga samaki kweli?

30/05/2016

Habari za sasa hivi,
leo naomba tujuzane ufugaji mseto wa samaki,mifugo na kilimo (mbogamboga).

INTEGRATED AQUACULTURE AND AGRICULTURE (IAA)
Ufugaji huu umeanza muda mrefu lakini wafugaji wengi huwa hawatumii. baada ya kuchimba bwawa la samaki na kukamilika jenga banda la kuku,bata juu yabwawa la samaki kwenye kona moja ya bwawa ambako kuna kina kifupi na eneo unapolishia samaki. kwa mifugo aina ya ng'ombe, mbuzi na wengine unaweza tengeneza mfereji mwembamba kutoka kwenye banda la mifugo kwenda kwenda kwenye bwawa la samaki. samadikutoka kwenye mifugo hutumika k**a chanzo cha mbolea ambayoinarutubishamaji kwenye bwawa lasamaki. Hii husaidia kuzalisha viluiluividogo vya jamii ya mimea (phytoplanktons) na wanyama (zooplanktons) ambavyo hutumika k**a chakula kwasamaki wafugwao. idadi ya wanyama watakao hitajika ilikurutubisha maji kwenye bwawa la samaki inategemea na ukubwa wa bwawa lako.Mfano:- bwawa lenye ukubwa wa mita 6*10M unaweza kuweka kuku/bata 10, ng'ombe mmoja, mbuzi/kondoo 3. ufgugaji huu husaidia kuhakikisha chakula ndani ya bwawa la samaki kuwa na chakula wakati wote. pia chakula cha aina hii kinakiasi kingi cha protini about (60%). Eneo karibu na bwawa la samaki linafaa kwa kilimo cha mbogamboga ambazo baadayamuda mfupi hukomaa na kuvuna ndani ya muda mfupi, mfano (bilinganya, hoho, mchicha, spinachi,bamia na mengineo). Maji kutoka kwenye bwawa la samaki hutumika kumwagilizia mbogamboga na kumbuk**aji hayo yana virtubisho vingi kutoka kwenye mbolea za wanyama ambavyo huhitajika na mimea kwa ukuaji.

ufugaji huu una faida mbalimbali
1. samaki
utapata mazao kutoka kwenye bwawa la samaki kwa kupata samaki

2. mbogamboga
hii husaidia kuongea mapato kwa mfugai na unaweza ukalima mchanganyiko wa mbogamboga nyingi kutokana na ukubwa wa eneo ululonalo.

3.malisho ya mifugo
mabaki mbalimbali kutoka kwenye mabaki ya mbogamboga hutumika k**a chakula kwa wanyama

4. ulinzi
kadri shughuli za uzalishaji zinavyozidi kuwa nyingi maeneo kuzunguka bwawa husaidia kulinda samaki wasishambuliwe na ndege pamoja naviumbe wengine ikiwemo binadamu ambao wanaweza kuwadhuru samakii kwa njia moja au nyingine.

5. matumizi mazuri ya rasilimali aridhi na maji
mseto wa shughuli hizi katika eneo moja husaidia kupunguza matumizii ya aridhi. Eneo dogo la aridhi linaweza kuzalisha mazao mbalimbali na mengi.

6. kupunguza uchafuzi wa mazingira
kwa ufugaji wa samaki wa aina hii husaidia maji kutoka kwenye bwwa la samaki kutoyaachia kwenda sehemu mbalimbali na kuchafua mazingira kutokana na vituvilivyomo ndani yake bali hutumika kumwagilizia mazao.

NOTE: inashauriwa kuweka mpira kwa ajili ya kufyonza maji kutoka kwenye bwawa la samaki ili kupunguza kuchafua maji ya bwawa. pia unaweza kutumia maji ya ndani ya bwawa la samaki kwa kumwagilizia wakati wowote muda wa ufugaji. kiasi cha maji ambayo yatapunguzwa ndani ya bwawa kwa ajili ya kumwagilizia mbogamboga inatakiwa kijazwe mara moja ili isijedhuru ukuajii wa samaki ndani ya bwawa la samaki.

leo nilipenda kushirikishana nanyi juu ya huu ufugaji mseto wa samaki, mifugo na kilimo. mapendekezo,nyongeza au maswali yanakalibishwa na sote kwa ujumla tutashiriki katika kujibu.

Naomba kuwasilisha
RealAquaculture

12/05/2016

somo linalofuata
UFUGAJI MSETO WA SAMAKI, KUKU NA MAZAO

Je!,unaelewaje juu ya ufugaji huu. toa maoni yako

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when REAL Aquaculture group posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to REAL Aquaculture group:

Share