18/10/2023
Rais wa Marekani, Joe Biden leo Jumatano, Oktoba 18, 2023 amewasili Nchini Israel akiwa chini ya ulinzi mkali kwa ajili ya kuzuru Taifa hilo lenye vita katika safari ya kidiplomasia ya hali ya juu.
Ziara yake inakuja siku moja baada ya mlipuko mbaya katika hospitali ya Gaza na kuua zaidi ya watu 500, kulingana na Wizara ya Afya ya Palestina.
Ikulu ya White House jana ilisema kwamba idadi ya vifo kutokana na shambulio la awali la Hamas nchini Israel imeongezeka hadi Wamarekani 31 waliouawa, huku Wamarekani 13 wakiwa bado hawajulikani waliko.