21/01/2026
: Serikali imebainisha kuwa imefanikiwa kuzuia kupanda kwa gharama za matumizi ya umeme kwa wananchi kwa kipindi cha miaka 10 tangu mwaka 2016, licha ya kuongezeka kwa bei za vifaa k**a nguzo na mita. Akizungumza Januari 21, 2026, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, ameeleza kuwa kiwango cha uunganishaji umeme nchini kimefikia asilimia 52, huku kukiwa na lengo la kufikia asilimia 75 ifikapo mwaka 2030 kupitia mipango mbalimbali ya nishati iliyosainiwa hivi karibuni.
Waziri Ndejembi ameongeza kuwa zoezi la ufungaji wa mita janja linaendelea nchi nzima ili kurahisisha upatikanaji wa umeme wa token bila kutumia vifaa vya ziada, huku miradi mikubwa ya njia za kusafirisha umeme mkoani Rukwa na mikoa ya Kusini ikiendelea kutekelezwa. Aidha, ujenzi wa miundombinu hiyo inalenga kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya uhakika na ya kuaminika kwa ajili ya kuchochea shughuli za maendeleo na huduma za kijamii kote nchini.
Kwa upande wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imepongeza jitihada za TANESCO na REA katika kutekeleza miradi mikubwa k**a ule wa Julius Nyerere (JNHPP) na miradi ya nishati ya jua. Mwenyekiti wa k**ati hiyo, Mhe. Subira Mgalu, amebainisha kuwa kuimarika kwa umeme kumesaidia kukuza uchumi na kuongeza mapato ya serikali, ambapo sekta za viwanda na migodi zimechangia TRA kufikia rekodi ya makusanyo ya Sh. trilioni 4.13 kwa mwezi mmoja.